JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI
YA RAIS- TAMISEMI
SHULE YA
SEKONDARI TUMAINI
S.L.P.533,
IRAMBA-SINGIDA
TAREHE,
14/06/2017
Simu:
0684534655/0762184451
Mkuu
wa shule:
Honoratha J. Mbiaji.
Barua
pepe: tumainisecondary1969@gmail.com
Blog:
tumainisecondary.blogsport.com
MZAZI/MLEZI WA MWANAFUNZI……………………………………………………
S.L.P………………………………………
YAH:
MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI TUMAINI HALMASHAURI YA IRAMBA
MKOA WA SINGIDA.
1. Nafurahi kukutaarifu
kuwa mwanao amechaguliwa kujiunga na kidato cha Tano katika shule ya sekondari
Tumaini iliyoko Wilaya ya IRAMBA katika mkoa wa SINGIDA mwaka 2017 tahasusi ya……………………………..
Shule iko kilomita
zipatazo 70 kutoka Singida mjini kando
kidogo mwa barabara itokayo Singida kwenda Mwanza. Kutoka Singinda kuna mabasi ya SIMANJIRO,KIRUMO na HIACE
ambayo huondoka Singida kati ya saa 6:30
na saa 7:00 mchana kila siku kwenda kiomboi na hupitia Kinampanda mahali shule
ilipo. Nauli ni shilingi 4,000/=. Endapo mwanao atapanda mabasi ya kutoka
Tabora, Nzega, Kahama, au Mwanza kwenda Arusha au Dar es salaam ashukie sehemu
iitwayo KITUSHA, kisha akodi
pikipiki hadi shuleni( km.8). Akifika Kitusha
kabla ya saa 7:00 mchana asubiri Basi inayotoka singida au Kiomboi
kupita Kinampanda. Shule ipo jirani na chuo cha ualimu Kinampanda.
Muhula wa masomo
unaanza tarehe 02/07/2017 Hivyo
mwanafunzi anatakiwa kuripoti shuleni
kuanzia tarehe 17/07/2017. Mwisho
wa kuripoti ni tarehe 31/07/2017.
2. MAHITAJI MUHIMU YA KUZINGATIA
2.1 Sare ya sahule
a) Sare
ya shule hii ni sketi bluu Bahari (light
blue) mbili(2), mshono wa Rinda bapa(box)mbele na nyuma, Mashati mawili(2) ya
mikono mirefu.
b) Rangi
ya hijab ( kijuba) ifanane na sare ya
shule, nusu kanzu nyeupe isiyobana mwili
pamoja na sketi ndefu rangi bluu bahari.
c) Viatu
vya shule ni vyeusi vya kufunga na kamba
vyenye visigino vifupi-Jozi mbili(2)
d) Soksi
jozi tatu nyeupe za shule.
e) Sweta
bluu Bahari yenye shepu ya V mbele.
f) Nguo
za kushindia(shamba dress)sketi nyeusi mbili,mshono marinda ya kutazamana na
T-shirt mbili(2) za kuvaa nje ya darasa( aje na shilingi 20,000/=)
g) Tai
mbili(2) rangi ya kufanana na kitambaa
cha sketi, iwe fupi yenye lastiki shigoni.
2.2 Ada na michango ya shule
a) Ada
ya shule kwa mwaka ni shilingi 70,000.00 kwa mwanafunzi wa bweni, mwanafunzi
anatakiwa kulipa shilingi 35,000.00 kwa muhula au kulipa ada yote kwa maramoja.
Fedha hizo zilipwe kwenye Akaunti ya shule Na.5061100179(Tumaini secondary
school Recurrent A/C)NMB (Tafadhali andika jina la mwanafunzi kwenye pay in
slip) aje nayo anaporipoti shule.
b)
Michango
inayotakiwa kulipwa na kila mzazi/mlezi.
i.
Shilingi 15,000/=kwa ajili ya ukarabati
wa samani
ii.
Shilingi 6,000/=kwa ajili ya
kitambulisho na picha
iii.
Shilingi 20,000/=kwa ajili ya taaluma
iv.
Shilingi 30,000/=kwa ajili ya kuwalipa
wapishi na walinzi na vibarua wengine
v.
Shilingi 2,000/=nembo ya shule
vi.
Shilingi 10,000/= kwa ajili ya huduma ya kwanza pamoja na Bima ya Afya.
vii.
shilingi 20,000/= mitihani ya kujipima
mock
viii.
shilingi 5,000/=fedha ya tahadhari
(haitarejeshwa)
NB: fedha za michango
mingine zilipwe kwenye a/c
no.50610005452-Tumaini secondary
school self reliance. Mwanafunzi aje na Bank paying slip original
yenye jina lake.
2.3
Mahitaji muhimu ambayo mwanafunzi anapaswa kuleta shuleni ni:-
2.3.1.Vifaa
vya darasani
(a)Madaftari makubwa 8(counter book) (b)
Kalamu za wino (c) Mathematical set
(d)Ream A4 moja ya karatasi kwa ajili ya
mitihani (e) Penseli(f) Rula
(g) Dictionary advanced learner
(h) Calculator-non programmable kwa Geography
na economics
(j) Aje na results slip (original),picha
nne passport size za wazazi au walezi
wanaoweza kukutembelea shuleni.
2.3.2.Vifaa vya kulalia
(a)Godoro (sponji) futi 2.5 inch 4 (b)Net ya
Mbu
(c)Mashuka mawili(2) light blue (e) Mto wenye foronya light blue (f)Blanketi 1
2.3.3.Vifaa
vya chakula
(a)Sahani (b) Bakuli (c) kijiko (d) kikombe
(e) chupa ya kuwekea maji ya kunywa
2.3.4.Vifaa
vya usafi binafsi
(a)Ndoo 2( lita 20 na lita 10) (b)Mswaki na dawa ya meno (c)Malapa (d)Sabuni
Za kufulia na kuogea.
(e)HKL-waje na jembe lenye mpini,HGK- Reki1
yenye mpini,HGE-Watering can
HGL -Panga lililonolewa,( Mifagio ya ndani(
soft broom) na mifagio ya nje
(Chelewa) ni
kwa wote.
Wako
katika ujenzi wa Taifa.
H.J.Mbiaji
MKUU
WA SHULE
SHULE
YA SEKONDARI TUMAINI.
MAKOSA
YANAYOWEZA KUMFUKUZISHA MWANAFUNZI SHULE
i.
Utoro
ii.
Wizi
iii.
Uasherati,
ushoga na ulawiti , Kuoa au kuolewa.
iv.
Kupata
ujauzito au kutoa mimba.
v.
Ulevi
au unywaji wa pombe na matumizi ya madawa ya kulevya .
vi.
Uvutaji
wa sigara au bangi.
vii.
Kuharibu
kwa makusudi mali ya umma.
viii.
Kupigana
mwanafunzi kwa mwanafunzi,kumpiga mwalimu au na mtu yeyote Yule.
ix.
Kudharau
Bendera ya Taifa
x.
Kulala
nje ya shule bila ruhusa ya Mkuu wa shule
xi.
Kutembelea
majumba ya starehe na nyumba za kulala wageni
xii.
Kugoma
kwa namna yoyote au kuchochea vurugu
xiii.
Kutoa
lugha ya matusi au lugha chafu kwa mwanafunzi,walimu,walezi,na jamii kwa
ujumla.
xiv.
Kumdharau
mwalimu, Kiongozi, Mfanyakazi na jamii kwa ujumla
xv.
Kutohudhuria
vipindi kwa uzembe
xvi.
Kutofanya
mitihani kwa makusudi/bila sababu ya msingi
xvii.
Kushirki
matendo ya uhalifu, siasa na matendo yoyote yale yanayovunja sheria za nchi.
xviii.
Kufanya
jaribio lolote la kujiua, au kutishia kujiua kama kunywa sumu n.k
xix.
Kumiliki
simu.
FOMU A:
WIZARA YA ELIMU SAYANSI,
TEKINOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
SHULE
YA SEKONDARI TUMAINI.
FOMU
YA KUKUBALI NAFASI ALIYOPEWA MWANAFUNZI
A.
|
i.
Jina kamili…………………………………………………………………….
ii.
Tarehe ya
kuzaliwa………………………..Wilaya……………………………
iii.
Dini……………………….Dhehebu………………………………………….
Mahali
atakapokuwa anaenda likizoni:
i.
Jina…………………………Uhusianao……………..Mahali……………..
ii.
Jina…………………………Uhusiano………………Mahali……………..
Kukubali
nafasi:
Mimi………………………………………nimeona
maelekezo ya kujiunga na shule ya Sekondari Tumaini. Nakubali kutimiza masharti
yote ya shule ikiwa ni pamoja na kutii sheria za shule. Nitakapokuwa shuleni,
nitajitahidi kwa uwezo wangu wote kusoma kwa bidii na kuchapa kazi za mikono
kwa bidii ili kutimiza lengo la kupata elimu katika ujumla wake.
Saini………………………..Tarehe………………………………………………………..
B.
|
i.
Jina kamili………………………………………………………………
ii.
Yeye ni mzazi au
mlezi…………………………………………………
iii.
Uhusiano uliopo na mwanafunzi……………………………………….
iv.
Kazi yake………………………………………………………………
v.
Anwani ya kazini………………………………………………………
vi.
Namba ya simu………………………………………………………….
vii.
Anwani ya
nyumbani………………………………………………………………
viii.
Uthibitisho wa Mzazi/Mlezi:
Nimehakikisha maelekezo na maagizo yameeleweka na
mtoto wnagu atafuata sheria na taratibu zote za shule ya sekondari Tumaini.
Jina……………………………………..Saini……………………Tarehe………………
FORM B:
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
REQUEST FOR MEDICAL EXAMINATION
PART A:
TO: The Medical Officer FROM: The Headmistress,
_______________________ Tumaini
Sec. School,
_______________________ P.O. Box
533,
_______________________
Kinampanda,
IRAMBA – SINGIDA.
DATE_____________
NAME________________________________
Please examine the above named person
as to her fitness for re-engagement as a
student in our school.
Signature _________________________
PART B: MEDICAL CERTIFICATE
(To be completed by
Medical Officer)
I have examined the above named
person ad consider that she is___________
______________________________________________________________
______________________________________________________________
Date______________________ Signature __________________________
Station____________________ Designation _______________________